Friday 24 February 2012

Laana yangu




Wadhani wanitambua
Hauning’amui hata

Waamini tabasamu hafifu ichezayo mdomoni
Huoni gubi la simanzi ilyofunikwa

Wahusudu mavazi yangu yanayonisitiri
Huoni vidonda vilivyofichwa ndani

Ukiona marafiki zangu wanavyojibeba kana kwamba dunia ni uridhi waliyopewa
Wadhani maisha yangu ni bahali shwari

Uonacho ni ngozi inayong’aa kwa kulishwa mafuta ya mikato
Hauelewi ati ngozi huo umodhoofika ndani

Mkwanja wangu ndio wewe waona
Hauelewi ukware wangu haukunipa hela tu- sonene pia niliongezewa

Hauamini rijali wa miraba minnne na umbo tisti kaanguswa na nyondenyonde
Ugonjwa huu haubagui

Waganguzi na waganga wameongea
Ugonjwa huu hausikii

Usihusudu maisha yangu
Tangu lini mzima akatamani uredi?

Mzee Varaq
My poems

No comments:

Post a Comment